Tuesday, May 1, 2012

FERGUSON AMTUHUMU MANCINI KUWABUGUDHI WAAMUZI.

KOCHA wa Manchester United, Sir Alex Ferguson amemtuhumu kocha Manchester City Roberto Mancini kwa kuwasumbua waamuzi baada ya makocha hao kugombana wakati wa mchezo baina ya timu hizo ulichezwa jana. Ferguson na Mancini ilibidi watenganishwe baada ya kushindwa kuzuia jazba zao kwa kunyoosheana vidole dakika ya ya 76 ya mchezo huo ambao City walifanikiwa kuibuka na ushindi wa bao 1-0. Ferguson alinyanyuka kutoka alipokuwa amekaa na kuanza kulalamika mchezo mbaya aliochezewa mshambuliaji wa timu yake Danny Welbeck na beki wa City Nigel De Jong. Kocha huyo ambaye ana miaka 70 alimtuhumu Mancini kuwabugudhi waamuzi katika kipindi chote cha msimu huu lakini akahoji kwanini kocha huyo hajalalamikia mchezo huo.

No comments:

Post a Comment