Monday, April 2, 2012

WENGER AKUNWA NA TAARABT.

KOCHA wa Arsenal, Arsene Wenger anaamini kiungo wa timu ya Queens Park Rangers, Adel Taarabt ana kila kitu cha kuitwa mchezaji bora lakini kwa sasa anahitaji kufanya vizuri zaidi kila wiki wakati timu yake ikicheza. Taarabt ndio alifunga bao lililoipa ushindi timu yake dhidi ya Arsenal Jumamosi kwenye Uwanja wa Loftus Road bao ambalo ni kwanza kwa mchezaji huyo katika msimu huu wa Ligi Kuu nchini humo. Mwanasoka huyo wa kimataifa wa Morocco, alikuwa chachu ya timu yake kupanda Ligi Kuu msimu uliopita, akiifungia mabao 19 na Wenger amesema kijana huyo mwenye umri wa miaka 22 sasa anatakiwa kudumisha ubora wake uwanjani. Wenger alimsifu kinda huyo kwamba ana kipaji cha hali ya juu na ameonyesha hilo kwenye mchezo huo lakini akasisitiza kuwa bado ana safari ndefu ya kuelekea mafanikio kwasababu anahitaji kucheza kwa kiwango cha juu mfululizo.

No comments:

Post a Comment