Monday, April 2, 2012

SIMBA WAONDOKA LEO KUIFUATA EL-SETIF.

WAWAKILISHI pekee wa Tanzania katika michuano ya Afrika, Simba SC wameondoka alfajiri ya leo Dar es Salaam kuelekea Algeria kwa ajili ya mechi ya marudiano, Raundi ya Pili Kombe la Shirikisho la Soka Afrika dhidi ya wenyeji ES Setif, wakipitia Algeria. Simba imeondoka nchini huku wakiwa na matumaini makubwa ya kuitoa ES Setif katika mchezo huo utakaofanyika Ijumaa wiki hii. Ofisa Habari wa Simba, Ezekiel Kamwaga alisema wachezaji wapo katika hali nzuri na kwamba wimbo wao ni ushindi, huku akiwataja viongozi watakaofuatana na timu hiyo kuwa ni Mwenyekiti wa klabu hiyo, Ismail Aden Rage, Mjumbe wa Kamati ya Utendaji ya klabu hiyo Damian Manembe na Kamwaga. Amesema benchi la ufundi watakaokuwepo ni Kocha Mkuu Milovan Cirkovic, Kocha Msaidizi Amatre Richard, kocha wa makipa James Kisaka, daktari wa timu Cosmas Kapinga, Nyagawa na mtunza vifaa Kessy Rajab. Aliwataja wachezaji waliopo kwenye msafara kuwa ni Juma Kaseja, Ally Mustafa, Nassor Masoud, Shomari Kapombe, Amir Maftaha, Juma Nyoso, Kelvin Yondani, Victor Costa, Obadia Mungusa, Jonas Mkude, Patrick Mafisango, Mwinyi Kazimoto, Haruna Moshi, Salum Machaku, Uhuru Suleiman, Felix Sunzu, Emmanuel Okwi, Edward Christopher, Derick Walulya na Gervais Kago.

No comments:

Post a Comment