Tuesday, April 24, 2012

FRANKFURT YAREJEA BUNDESLIGA BAADA YA KUPOROMOKA MSIMU ULIOPITA.

KLABU ya Eintracht Frankfurt imefanikiwa kurejea katika Ligi Kuu nchini Ujerumani wakiungana na timu ya Greuther Fuerth kama timu mbili ambazo zimepanda daraja kutoka daraja la pili zilipokuwa. Hakuna timu yoyote kati ya Frankfurt au Fuerth ambazo zinaweza kuondolewa katika nafasi hizo mbili za kupanda daraja baada ya timu hizo kuongoza kwa lama nane ambazo haziwezi kufikiwa na timu nyingine katika msimamo wa ligi hiyo. Kocha Mkuu wa Frankfurt, Armin Veh ambaye alichukua mikoba ya kuinoa klabu hiyo wakat iliposhuka daraja msimu uliopita amesema kuwa anahitaji muda ili kujua hatma yake huko mbele baada ya kuiwezesha klabu hiyo kurejea Bundesliga. Hatahivyo Mkurugenzi wa klabu hiyo amesema kuwa anaamini kuwa Veh mwenye umri wa miaka 51 ambaye amewahi kuvinoa vilabu vya VFB Stuttgart, Wolfsburg na SV Hamburg kwamba atasaini mkataba mpya na klabu hiyo.

No comments:

Post a Comment