Tuesday, April 3, 2012

BEKI WA ATALANTA AKAMATWA KWA KASHFA YA UPANGAJI MATOKEO.

BEKI wa Atalanta, Andrea Masiello amekamatawa baada ya taarifa kwamba alihusika na upangaji wa matokeo na wachezaji wenzake wanane wa zamani wa Bari na suala lao lipo chini ya uchunguzi. Taarifa iliyotolewa na Shirikisho la Soka Italia imesema kuwa upangaji wa matokeo unazorotesha maendeleo ya soka nchini humo na wameahidi kuchukua hatua kwa atakayekutwa na hatia. Tangu kundi la kwanza la watu 16 wakamatwe Juni, mwaka jana, watu wengine 30 wamekamatwa, akiwemo nahodha wa zamani wa Atalanta, Cristiano Doni na nahodha wa zamani wa Lazio, Giuseppe Signori. Mechi tisa za mwisho za Bari msimu uliopita zinachunguzwa, kwa mujibu wa shirikisho, ikiwemo mechi ambayo bao la kujifunga la Masiello liliisaidia Lecce kushinda 2-0 na kuepuka kushuka daraja, baada ya Bari kuwa tayari imeshuka.

No comments:

Post a Comment