Tuesday, April 3, 2012

SAFA YAZIDAI MIJI WENYEJI WA AFCON RANDI MILIONI 22.

CHAMA cha Soka nchini Afrika Kusini-SAFA kinadai kiasi cha randi milioni 22 kwa kila mji utakaotumika kama mwenyeji wa mashindano ya Kombe la Mataifa ya Afrika itakayofanyika mwakani. SAFA kinatafuta fedha kwa ajili ya kufidia gharama ya michuano hiyo ambayo inatarajiwa kutumia kiasi cha zaidi ya randi milioni 100 ambapo miji hiyo saba itakayokuwa mwenyeji itatakiwa kulipa kiasi hicho au watanyimwa nafasi hiyo. Suala hili lilijulikana baada ya jiji la Cape Town kutaka kujitoa katika kinyang’anyiro cha kuwa mwenyeji kwasababu hawataki kutumia pesa za walipa kodi wao kwa ajili mpira. Diwani wa jiji la Cape Town Grant Pascoe amesema mji wake huo una nia ya kuwa mwenyeji wa michuano hiyo ndio maana wametuma barua ya maombi lakini kwa kiwango ambacho SAFA wanadai hawataweza kukimudu.

No comments:

Post a Comment