Sunday, April 22, 2012

GUARDIOLA AWAPONGEZA MADRID.

KOCHA wa Barcelona Pep Guardiola amewapongeza Real Madrid kama mabingwa wapya wa Ligi Kuu nchini Hispania baada ya kikosi chake kufungwa mabao 2-1 na mahasimu wao hao katika Uwanja wa Camp Nou jana. Kipigo kinaifanya Madrid kuongoza ligi hiyo kwa alama saba huku wakiwa wamebakiza michezo minne na kukaribia kunyakuwa taji hilo ambalo wamelikosa toka mwaka 2008 huku katika historia wakiwa wamelinyakuwa mara 32. Guardiola alikisifu kikosi cha Madrid kwa ushindi huo ambao amesema kuwa hana shaka kuwa watanyakuwa taji la ligi ingawa pia alikisifu kikosi chake kwa kucheza soka safi lakini bahati haikuwa yao safari hii. Kwasasa Barcelona inabidi wajipange upya kwa ajili ya mchezo wao wa nusu fainali Ligi ya Mabingwa Ulaya dhidi ya Chelsea ambapo itabidi watafute ushindi wowote baada ya kufungwa bao 1-0 katika mchezo wa kwanza.

No comments:

Post a Comment